Tuesday, June 17, 2025
spot_img

TFF KUTAJA MSHIRIKA MPYA WA MICHEZO YA KUBASHIRI KWA MSIMU WA 2025/26

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kuwa kuanzia msimu ujao wa 2025/2026, litakuwa na mshirika rasmi wa michezo ya kubashiri kwa ajili ya mashindano yote yanayosimamiwa na shirikisho hilo.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF, mshirika huyo atapewa haki ya kipekee ya kutoa huduma za kubashiri kwa kipindi chote cha makubaliano. Hii ina maana kuwa taasisi au kampuni yoyote itakayohitaji kuweka “odds” (alama za ubashiri) kwa mechi zitakazokuwa chini ya TFF, italazimika kuwasiliana moja kwa moja na mshirika huyo.

TFF imesisitiza kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza usimamizi bora wa taarifa za mechi, kuongeza mapato ya mashindano, na kuhakikisha mashirikiano yenye manufaa kwa pande zote — wachezaji, vilabu, wadhamini, na mashabiki.

Majina ya kampuni au taasisi zitakazoshiriki katika mchakato wa kupata nafasi hiyo ya ushirika yanatarajiwa kutangazwa hivi karibuni baada ya kukamilika kwa taratibu za kisheria na kiutawala.

Zinazihusiana

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Ungana Nasi Kupitia

0FansLike
0FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Za hivi karibuni