Home Kitaifa Chalamila ataka barabara Ubungo-Kimara ikamilike haraka

Chalamila ataka barabara Ubungo-Kimara ikamilike haraka

0

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila amemtaka mkandarasi anayejenga barabara ya Morogoro kipande cha Ubungo -Kimara kukuongeza kasi ya ujenzi ili kupunguza msongamano wa magari.

Chalamila alitoa wito huo Aprili 10,2025 ikiwa ni siku ya pili ya ziara ya kukagua hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi Wilaya ya Ubungo na kutoa maagizo kwa viongozi wa halmashauri pamoja na wakandarasi kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

“Haiwezekani kutoka pale ubungo mpaka Kimara utumie saa nne wakati kila siku tunavutia biashara masaa 24 na hiyo itakuwa siyo ufanisi wa kazi hivyo naomba ninyi Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) na wakandarasi kufahamu umuhimu wa barabara hii kwani inatumika na magari mengi kwenda mikoa yote,”amesema Chalamila.

NO COMMENTS

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Exit mobile version