Monday, December 15, 2025
spot_img

TANZANIA YAREJESHA RAIA WAKE KUTOKA ISRAEL

KATIKA hali inayoashiria bado hali si shwari katika vita vya Israel na Iran-hatimaye taifa la Tanzania limewarejesha baashi ya raia wake waliokuwa Israel kuhofia hali ya usalama kutokana na mapigano yanayoendelea dhidi ya Iran.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei

Kwa undani fuatilia ripoti hii ya Trigen Media

Mataifa yaliyo mengi duniani yalichukua hatua ya kuwaondoa Raia wake kwa kile kilichoelezwa kuwa ni hali ya hatari kwao kufuatia vita kati ya   Israel na Iran ambavyo vimeendelea kwa zaidi ya siku 10 hadi sasa.

Shughuli za Uokoaji na kuondoa vifusi vilivyotokana na mashambulizi ya Iran huko Israel.Picha na mitandao ya kimataifa

Hata hivyo pamoja na Rais Trump kukaririwa akisema kuwa vita imesitishwa lakini bado hali ni tete na lolote lawesa kutokea kwa pande hizo mbili.

Kati ya watanzania waliorejeshwa Baadhi yao ni wale waliokuwa wakifanya kazi- wanafunzi, na na wale waliokwenda kwaajili ya matibabu.

Wakizungumza huku wakisitasita kutokana na khofu, Hanifa Rashid Abass na Amina Soud waliorejea nyumbani wakitokea nchini Israel wanaelezea wasiwasi waliokuwa nao katika kipindi kigumu cha vita.

Mataifa haya mawili yanayopigana ni rafiki wa Tanzania na kumekuwa na mwingiliano mkubwa katika nyanja mbali mbali kama vile za kijamii-kichumi na matibabu.

Zinazihusiana

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Ungana Nasi Kupitia

0FansLike
0FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Za hivi karibuni