Aliyekuwa Mwandishi wa Habari na Mtangazaji wa Radio Kwizera FM ya Ngara, Juventus Juvenary Illambona maarufu kama Juveilla, hatimaye amejitosa katika siasa na kutangaza kuwania rasmi Udiwani wa Kata ya Kibimba, wilayani Ngara kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Illambona aliieleza Trigen kwamba amefikia uamuzi huo baada ya tafakari ya kina, akilenga kuleta maendeleo kupitia uzoefu wake katika mawasiliano na utetezi wa jamii.

Miongoni mwa vipaumbele vyake ni: Pamoja na Kuboresha miundombinu ya barabara, maji na umeme,
Kuweka utawala wa uwazi na ushirikishwaji wa wananchi, Uwezeshaji wa vijana, wanawake na walemavuKukuza michezo na sanaa,
Kutumia rasilimali kama mto Ruvubu na uwanja wa ndege wa Ruganzo kwa maendeleo ya kiuchumi.

Amesema atachukua fomu ya kugombea tarehe 28 Juni 2025, na kuomba wananchi wa Kibimba na watu wenye mapenzi mema kumuunga mkono katika safari yake ya kisiasa.