Tuesday, June 17, 2025
spot_img

MILLEN MAGESA KUANDAA MISS UNIVERSE TANZANIA 2025

BARAZA la Sanaa la Taifa(BASATA) limetoa baraka na kibali kwa Mwanamitindo wa Kimataifa na Mrembo wa Tanzania, Millen Happiness Magese, kupitia kampuni yake ya MILLEN PRIVÉ & Co. LIFESTYLE Bespoke Luxury Lifestyle & Hospitality Management kuandaa mashindano ya Miss Universe Tanzania.

Millen amepata baraka na kibali cha kuandaa Miss Universe Tanzania jijini Dar es Salaam, ambapo wadau wa tasnia ya ulimbwende akiwemo Miss Universe mwaka 2024, Judith Ngussa wameahidi kutoa kila aina ya ushirikiano kwa Millen kuhakikisha mashindano hayo yanafanikiwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Dkt. Kedmon Mapana, amesema baraza hilo kama walezi na wasimamizi wa karibu wa tasnia ya urembo,ulimbwende na utanashati wameamua kumpa baraka zote Millen Happiness Magese kuandaa mashindano hayo nchini.

“Tunajivunia na wale wanaofuatilia Millen Happiness Magese yuko nje ya nchi anakaa Marekani, lakini bado moyo wake unasema kwanini asirudi nyumbani afanye jambo kwa maendeleo ya nchi yetu ya Tanzania, lakini pia kwa maendeleo na ustawi wa Baraza la Sanaa la Taifa.

“Hivyo tunamtakia kila la heri na tunategemeo mambo yetu yatakuwa mazuri kwamba kazi hii Millen unaiweza lakini na sisi kama Tanzania tutafurahi kuona mashindano ya ulimbwende Miss Universe tuna Mwakilishi kutoka Tanzania,”amesema Dk.Mapana.

Aidha amesema mashindano ya Miss Universe yana mambo mengi na ndio maana mbali ya kumpatia baraka na kibali cha kuandaa mashindano hayo wamemkabidhi muongozo wa maadili katika kazi za sanaa na kusisitiza wanapofanya mashindano ya ulimbwende wasisahau kuna mila na desturi zetu.

“Tuhakikishe kwamba kama Tanzania tunapokwenda huko nje tunasema huyu mrembo anatoka Tanzania na anapambanua vipi hasa suala la maadili , hivyo tunatarajia muongozo huu ambao tumekukabidhi Millen utautumia vizuri na sisi BASATA tutahakikisha jambo hili linakwenda kutekelezeka vizuri.

Kwa upande wake Millen Happiness Magese ameishukuru BASATA kumpatia baraka na kibali cha kuandaa mashindano ya Miss Universe Tanzania yeye kupitia kampuni yake kuratibu.

“Nashukuru kwa kupata kibali cha Miss Universe Tanzania kutoka Miss Universe Organization na kwa sasa pia nimepata kibali cha hapa Tanzania kupitia BASATA ,Kwahiyo nina baraka zote mbili.Kwa kushirikiana na BASATA na wadau wote nchini tunategemea safari hii itakuwa ni suala nzima la kunyanyua hii Sanaa nzima ya mambo ya ulimwende Tanzania.

“Nawashukuru kwa kutupa nafasi hii ,kwetu ni nafasi muhimu kwani tutatumia platform hii ya Miss Universe kuitangaza nchi yetu kwani watu zaidi ya bilioni moja kwa wakati mmoja hufuatilia na nchi zaidi ya 174 zimekuwa zikishiriki mashindano haya,”amesema Millen.

Zinazihusiana

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Ungana Nasi Kupitia

0FansLike
0FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Za hivi karibuni