Tuesday, June 17, 2025
spot_img

DKT TULIA ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO JIPYA LA UYOLE MKOANI MBEYA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Dk. Tulia Ackson, ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge katika jimbo jipya la Uyole, mkoani Mbeya, katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Akizungumza leo Mei 23, 2025, wakati wa Mkutano Mkuu Maalum wa Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Tulia amesema amefikia uamuzi huo baada ya kuona kasi ndogo ya maendeleo katika eneo hilo, hali inayowalazimu wananchi kusubiri kwa muda mrefu kupata huduma stahiki.

Akitumia nafasi hiyo kuomba ridhaa ya wanachama wa CCM, Dk. Tulia amewahimiza viongozi na wanachama kuchagua kiongozi atakayekuwa mtumishi wa kweli wa wananchi na si mtu wa kutafuta maslahi binafsi.

Jimbo la Uyole ni miongoni mwa majimbo mapya yaliyoundwa katika marekebisho ya mipaka ya kisiasa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, na linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na idadi ya wakazi na umuhimu wake kiuchumi ndani ya Mkoa wa Mbeya.

Zinazihusiana

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Ungana Nasi Kupitia

0FansLike
0FollowersFollow
0SubscribersSubscribe
- Advertisement -spot_img

Za hivi karibuni